Wednesday, 29 June 2016

Imeandaliwa na:  Jalilu Zaidi;

                      Barua Pepe: jaliluzaid@gmail.com 
                      WhatsApp: +255656587011.

Habari ndugu msomaji na Mtanzania mwenye uzalendo na Taifa lake na mwenye dhamira ya wazi kabisa kuona kila kitu kinachomilikiwa na Tanzania kinaweza kupiga hatua na kusonga mbele zaidi ikiwemo Michezo, Muziki, Elimu, Nidhamu, Usalama, Amani, Demokrasia, Miundombinu, Lugha ya Taifa pamoja na mambo mengine mengi yanayopatikana kwenye Nchi yetu tuipendayo ya Tanzania. Kwanza kabisa nianze na maneno ya   Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage  Nyerere ambae  ametuasa tusiwe wabinafsi katika masuala yahusuyo taifa.   Suala la ubinafsi amelipiga vita tangu alipoasisi taifa hili na kutuagiza tuondokane na ubinafsi kama alivyoandika katika kitabu chake cha ‘Tujisahihishe.’ Kitabu hiki kilichapishwa mwezi wa  Juni ya mwaka wa  1962. Kwa maana hiyo, alitupa fursa ya kuielimisha jamii bila uchoyo na husuda kupitia njia mbali mbali ikiwemo Mikutano ya hadhara, Semina na Mikusanyiko ya Hadhara mbali mbali ili kuielimisha jamii ya Kitanzania. 
Njia nyingine raisi ambayo watu wengi tunaweza kujivunia sasa hivi kuna mitandao mingi ya kijamii ikiwemo tovuti mbali mbali Mfano;  jaliluzaid.com , chahali.com , millardayo.com , teknokona.com na nyingine nyingi  ambazo zinasaidia kwa kiasi kikubwa kuelimisha jamii na kuhabarisha pia jamii kwa lugha yetu ya Taifa ya Kiswahili maana kupitia kuhabarika jamii inapata kufahamu fursa mbali mbali za kimaendeleo hapa nchini na nje pia ya Nchi.

Monday, 20 June 2016

Kama ilivyo ada, #ElimikaWikiendi iko kwaajili ya kila mzungumza Kiswahili ili apate fursa ya kuelimika na kuwaelimisha wengine. Kuanzia sasa, matangazo yote ya vipindi vyote vitakavyokuwa vinakuja kupitia 'Twitter' ama matangazo ya kawaida kwako mzungumza Kiswahili yatakuwa yakiwekwa hapa. Usikose kupitia kila siku ili kuelimika zaidi na kuendelea kuwashirikisha ndugu, jamaa na marafiki ili nao waweze kuelimisha na kuelimishwa. Karibu sana, #ElimikaWikiendi ni zaidi ya Darasa!!!
                                                     







Kutoka Twitter

Zilizo Maarufu

Tangaza Nasi

Tangaza Nasi

Tuachie Ujumbe