Habari ndugu msomaji na Mtanzania mwenye
uzalendo na Taifa lake na mwenye dhamira ya wazi kabisa kuona kila kitu
kinachomilikiwa na Tanzania kinaweza kupiga hatua na kusonga mbele zaidi
ikiwemo Michezo, Muziki, Elimu, Nidhamu, Usalama, Amani, Demokrasia, Miundombinu,
Lugha ya Taifa pamoja na mambo mengine mengi yanayopatikana kwenye Nchi yetu
tuipendayo ya Tanzania. Kwanza kabisa nianze na maneno ya Hayati
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambae ametuasa
tusiwe wabinafsi katika masuala yahusuyo taifa. Suala la ubinafsi
amelipiga vita tangu alipoasisi taifa hili na kutuagiza tuondokane na ubinafsi
kama alivyoandika katika kitabu chake cha ‘Tujisahihishe.’ Kitabu hiki
kilichapishwa mwezi wa Juni ya mwaka wa 1962. Kwa maana hiyo,
alitupa fursa ya kuielimisha jamii bila uchoyo na husuda kupitia njia mbali
mbali ikiwemo Mikutano ya hadhara, Semina na Mikusanyiko ya Hadhara mbali mbali
ili kuielimisha jamii ya Kitanzania.
Njia nyingine raisi ambayo watu wengi
tunaweza kujivunia sasa hivi kuna mitandao mingi ya kijamii ikiwemo tovuti
mbali mbali Mfano; jaliluzaid.com , chahali.com , millardayo.com , teknokona.com na nyingine nyingi
ambazo zinasaidia kwa kiasi kikubwa kuelimisha jamii na kuhabarisha pia
jamii kwa lugha yetu ya Taifa ya Kiswahili maana kupitia kuhabarika jamii
inapata kufahamu fursa mbali mbali za kimaendeleo hapa nchini na nje pia ya
Nchi.